Maziko ya mtoto albino aliyekatwa viungo vyake kufanyika chini ya ulinzi mkali leo saa 5 asubuhi katika Kijiji cha Ibondo | HABARI MATUKIO TEKNOLOJIA NDANI NA NJE YA Tz

Maziko ya mtoto albino aliyekatwa viungo vyake kufanyika chini ya ulinzi mkali leo saa 5 asubuhi katika Kijiji cha Ibondo

Mtoto mwenye ulemavu wa ngozi, Yohana Bahati (1), aliyetekwa juzi katika Kijiji cha Ilelema, wilayani Chato mkoani Geita na kuokotwa katika Hifadhi ya Biharamulo akiwa amekufa bila mikono wala miguu, atazikwa leo saa 5 asubuhi katika Kijiji cha Ibondo, mkoani Geita chini ya ulinzi mkali wa polisi.
Yohana alitekwa nyumbani kwao saa mbili usiku, akiwa amebebwa na mama yake. Tukio la kutekwa mtoto huyo lilifanywa na watu wawili, ambao pia walimjeruhi mama huyo kwa kumkata mapanga kichwani.
Kamanda wa Polisi mkoani Geita, Joseph Konyo alisema juzi kuwa mwili wa mtoto huyo ulikutwa kwenye shamba la mahindi katika Kijiji cha Kimasa.
 Alisema mwili huo uliokotwa juzi Februari 17, saa 12 jioni kwenye makazi yasiyo rasmi.
Ndugu wa marehemu, walisema kuwa  Kamanda Konyo ameahidi kutoa ulinzi mkali wakati wa mazishi hayo kutokana na mazingira ya tukio lenyewe.
Katika hatua nyingine, hali ya mama wa mtoto mwenye ulemavu wa ngozi, ambaye alitekwa na kufariki dunia baada ya kukatwa viungo, imeelezwa kuanza kuimarika na kwamba kwa sasa ameanza kuzungumza polepole pamoja na kula.
Mama huyo, Esther Jonas (30), ambaye alifanyiwa upasuaji wa kichwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando, hali yake imeanza kuimarika baada ya kuanza kupumua vizuri tofauti na alivyokuwa jana na kwamba bado madaktari wanaendelea kumpa matibabu.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jana, Mkuu wa Kitengo cha Dharura BMC, Dk Derick David alisema hali ya mama huyo kwa sasa imeanza kuwa nzuri tofauti na jana.
“Ninachoweza kusema kwa leo (jana), hali ya mfiwa imeanza kuimarika na ameanza kupumua vizuri na kuzungumza polepole,” alisema Dk David
SHARE

Unknown

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment