Jokate: Sipendi Kutomaswa Kwenye Filamu za Mambo ya Mapenzi! | HABARI MATUKIO TEKNOLOJIA NDANI NA NJE YA Tz

Jokate: Sipendi Kutomaswa Kwenye Filamu za Mambo ya Mapenzi!




Mwanamitindo na mwigizaji wa filamu, Jokate Mwegelo amesema kuwa hapendi kuigiza sini za mapenzi hasa zile anazotakiwa kushikwashikwa na mwanaume hasa asiyemjua.
 
Jokate alifunguka hayo wakati paparazi wa GPL alipotaka kujua namna ambavyo wazazi na mpenzi wake wanavyolipokea suala la yeye kuigiza sini za kushikwashikwa na wanaume tofauti katika filamu ndipo alipofunguka kuwa suala hilo limekuwa likipigwa vita na wazazi wake lakini analazimika kufanya kwa sababu ndiyo kazi aliyoichagua.
 
“Wazazi wangu wanachukia sana jambo hili na huwa wanasema bora niache filamu, hata mimi mwenyewe huwa sipendi ila huwa navumilia kwa kuwa ni kazi, sina jinsi,” alisema Jokate.
SHARE

Unknown

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment