Mwenyekiti wa vijana waliopata mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) waliokuwa wakitaka kufanya maandamano kwenda ikulu atekwa | HABARI MATUKIO TEKNOLOJIA NDANI NA NJE YA Tz

Mwenyekiti wa vijana waliopata mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) waliokuwa wakitaka kufanya maandamano kwenda ikulu atekwa

Mvutano mkubwa umeibuka kati ya Jeshi la Polisi na vijana waliopata mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kufuatia kupotea kwa Mwenyekiti wao wa Vijana, George Mgoba, katika mazingira ya utatanishi.
Hata hivyo, viongozi wa vijana hao wamehojiwa kwa zaidi ya saa nane katika kituo cha polisi kati kwa kile polisi walichokiita walikuwa wakizungumza nao kuhusu madai yao.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Makamu Mwenyekiti wa Askari hao, Parali Kiwango, alisema mwenyekiti wao alipotea Jumatatu, majira ya saa ya saa 3:00 nyumbani kwake Mabibo Royola. Alisema tangu siku atoweke, hawana mawasiliano naye baada ya namba za simu zake za mikononi kuwa zimezimwa.
Kiwango alisema kwa mujibu wa mke wake, Mgoba alipigiwa simu na mtu ambaye hajafahamika akimtaka wakutane eneeo la Mabibo mwisho, alipoondoka hakurejea tena.
“Kwa mujibu wa mke wake anasema mtu huyo alijitambulisha kwa askari mwenzake, lakini sisi hatukumpigia simu ya aina hiyo, tunajua vyombo vya usalama vimehusika,” alisema Kiwango
Vijana hao waliomaliza mafunzo yao ya kijeshi katika kambi mbalimbali za JKT nchini, wamekuwa wakidai kupewa ajira kulingana na mafunzo waliyopewa.
Hata hivyo, wametishia kuitisha maandamano ya siku tatu yatakayoishia Ikulu ili kumshinikiza Rais Jakaya Kikwete kusikiliza kilio chao.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, akizungumza ofisini kwake, alikana jeshi hilo kuhusika na kupotea kwa Mgoba na aliahidi kutoa kauli kuhusu suala muda utakapofika.
Viongozi wa vijana hao wamehojiwa na polisi kwa muda wa saa tisa kwa kile kinachoelezwa kuzima jaribio la mandamano.
Akizungumza mara baada ya kikao hicho, Kiwango alisema walihojiwa na maafisa wa ofisi ya Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kuhusu madai ya wao kutaka kuandamana.
Alisema mahojiano hayo yalianza kufanyika kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi majira ya saa 7:00 mchana na kupewa mapumziko mafupi na illipofika saa 8:00 waliitwa Ofisi ya Kova na kuhojiwa hadi saa 10 jioni walipoachiwa.
“Kiujumla sisi tulitoa maelezo yetu kwa nini tunataka kuandamana, lakini tuliwaambia watuonyeshe mwenyekiti wetu na wamuachie haraka,” alisema
SHARE

Unknown

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment