Kina Warioba walipwa kiinua mgongo Sh640 mil | HABARI MATUKIO TEKNOLOJIA NDANI NA NJE YA Tz

Kina Warioba walipwa kiinua mgongo Sh640 mil

“Ni mwaka mzima umepita tangu tumalize kazi yetu. Wajumbe wa tume hawakwenda kufanya kazi ya kuandaa rasimu kwa ajili ya kutafuta fedha.” 
Serikali imeanza kulipa kiinua mgongo kwa wajumbe wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Wariona na jumla ya Sh640 milioni zitalipwa kwa watu 32.
Tume hiyo, ambayo ilifanya kazi ya kukusanya maoni na kuandika rasimu mbili za Katiba kwa miaka miwili, iliwasilisha ripoti yake kwenye Bunge Maalumu la Katiba mwezi Machi mwaka jana, ikiwa ni kutimiza kifungu cha 31 (1) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.
Rais Jakaya Kikwete alisema kuwa anafikiria kuwalipa wajumbe wa tume hiyo aina fulani ya kifuta jasho ambacho kiwango chake atakiamua yeye na kwa wakati mwafaka na kulingana na rasilimali za Serikali.
Habari ambazo paparazi imezipata zinasema kuwa wajumbe wa kamati hiyo wanalipwa Sh20 milioni kila mmoja, tofauti na habari zilizokuwa zimezagaa kuwa kila mjumbe angelipwa Sh200 milioni.  Uchunguzi wa paparazi umebaini kuwa mbali na wajumbe hao, makamishna wapatao 30 na viongozi wao wawili kutoka Bara na Visiwani walioshirikiana na tume kufanya kazi hiyo, wamo kwenye mpango huo, lakini inaonekana baadhi ya wajumbe hawajaridhika na kiwango hicho.
“Pamoja na kumshkuru Rais Kikwete kwa kufanikisha malipo yetu ya mafao, bado naona kiwango tulicholipwa ni kidogo kutokana na ukubwa wa kazi na uzito wake,” alisema mmoja wa makamishna ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe.
Alisema kwamba wakati wakisubiri kulipwa mafao yao kwa takriban mwaka, walikuwa na matumaini makubwa ya kulipwa kiasi cha Sh35 milioni kila mmoja kutokana na kazi kubwa waliyoifanya.
Hata hivyo, Jaji Warioba alisema wakati wanakubali kufanya kazi hiyo, hawakuwa na tamaa ya fedha na kwamba kama kuna malalamiko, basi ni ya mtu binafsi na siyo tume.
Alisema Rais alipewa uwezo wa kisheria kupanga na kuamua viwango vya kulipwa mafao viongozi wa tume hiyo baada ya kukamilisha kazi kwa jinsi atakavyoona inafaa.
Alisema kuwa hata barua zao za uteuzi zilisema watakuwa wakilipwa kiasi fulani wakiwa kazini na wakimaliza kazi, Serikali itawalipa kiinua mgongo kwa jinsi Rais atakavyoamua.
“Hivi karibuni Serikali ilinieleza kuwa italipa fedha hiyo na mimi nikawaeleza wajumbe. Sikuwa nikipata malalamiko kwamba wanategemea kiasi gani. Wapo ambao walikuwa wamesahau kabisa kuwa kuna malipo hayo,” alisema.
“Mimi kama mwenyekiti wao najua wajumbe hawakuwa na tamaa ya fedha na kama kuna malalamiko yoyote basi ni ya mtu mmoja lakini siyo tume.”
SHARE

Unknown

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment